Wasafwa

Wasafwa ni kabila la watu jamii ya Wabantu kutoka eneo la milima ya mkoa wa Mbeya, kusini mwa nchi ya Tanzania.

Wako hasa katika wilaya za Mbeya mjini, Mbeya vijijini, Mbozi na Chunya

Mwaka 1987 idadi ya Wasafwa ilikadiriwa kuwa 158,000 [1].

Lugha yao ni Kisafwa, lugha yenye uhusiano wa moja kwa moja na Kibantu. Salamu yao kuu ni "Mwagona".

Rangi kuu ya mavazi yao ni njano.

Dini kuu iliyotawala kati yao ni Ukristo, lakini wengine wamebaki kuamini mila zao.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search