Akili

Akili (kwa Kiingereza "intelligence") ni kipawa kinachowezesha kufikiri, kuelewa, kuwasiliana, kujifunza, kupanga na kutatua matatizo. Ni ufahamu uliomo katika ubongo wa binadamu, unaoweza hata kutofautisha jambo kwa wema na ubaya wake na hatimaye kumuongoza katika kufanya maamuzi.

Ingawa akili kwa ujumla hutumiwa kuhusiana na binadamu, baadhi ya wanyama kama sokwe, bonobo, mbwa [1] n.k. na hata mimea [2] [3] huwa na dalili fulani za akili.

Dhana kuhusu asili ya akili zinatofautiana.

Akili bandia ni akili ya mashine inayopatikana kwa kutumia programu za kompyuta.

  1. "The Intelligence of Dogs".
  2. "Green plants as intelligent organism".
  3. "Mindless mastery".

© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search