Amerika

Amerika duniani

Amerika ni jina la mabara mawili makubwa upande wa magharibi wa Afrika na Ulaya.

Amerika iko kati ya Bahari ya Atlantiki na Bahari ya Pasifiki kwa urefu wa kilomita 15,000 kutoka kaskazini (rasi Columbia) hadi kusini (rasi Hoorn).

Eneo lote ni km² 42,000,000 na jumla ya wakazi ni milioni 800.

Ramani ya Amerika yote

Eneo hugawiwa katika sehemu tatu au mbili, yaani ama

ama

Hesabu ya pande tatu inalingana na jiografia inayotambua hasa mabamba matatu yanayobeba sehemu hizi tatu: Amerika ya Kaskazini hulala hasa juu ya Bamba la Amerika ya Kaskazini, Amerika ya Kati juu ya Bamba la Karibi na Amerika ya Kusini hasa juu ya Bamba la Amerika ya Kusini.

Katika hesabu ya mabara mawili kwa kawaida Amerika ya Kati huhesabiwa kuwa sehemu ya Amerika Kaskazini. Kumbe upande wa utamaduni Amerika ya Kati na ya Kusini kwa pamoja huitwa "Amerika ya Kilatini" kutokana na lugha na utamaduni wa Kihispania na wa Kireno zilizofinyanga tabia za mataifa yake.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search