Bahari ya Karibi

Ramani ya Amerika ya Kati na Bahari ya Karibi

Bahari ya Karibi ni bahari ya pembeni ya Atlantiki iliyoko kusini ya Ghuba ya Meksiko. Upande wa magharibi imepakana na Amerika ya Kati, kusini na Amerika ya Kusini. Pinde la Visiwa vya Karibi linaitenga na Atlantiki yenyewe.

Bahari ya Karibi ina eneo la 2,754,000 km². Inafunika sehemu kubwa ya bamba la Karibi. Kina kikubwa kipo katika mfereji wa Kayman kati ya visiwa vya Kuba na Jamaika mwenye urefu wa 7,686 m chini ya UB.

Kuna hori za bahari na ghuba mbalimbali kama ghuba ya Venezuela na ghuba ya Honduras.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search