Bakteriofagi (pia fagi au vilabakteria) ni virusi zinazoambukiza na kujinakili ndani ya bakteria na arkea. Jina hilo linatokana na "bakteria" na neno la Kiyanuni φαγεῖν (fagein), yaani "kula". Bakteriofagi zimeundwa kwa protini ambazo zina jenomu ya ADN au ARN ndani yao, na zinaweza kuwa na miundo ama sahili ama changamano. Jenomu zao zinaweza kusimba jeni chache kama nne (k.m. MS2) au jeni nyingi kama mamia. Fagi hujinakili ndani ya bakteria kufuatia uingizaji wa jenomu zao kwenye sitoplazimu ya bakteria[1].
Bakteriofagi ni kati ya viumbe vya kawaida na anuwai sana katika tabakaviumbe. Bakteriofagi ni virusi za kila mahali zinazopatikana mahali popote bakteria walipo. Inakadiriwa kuna zaidi ya bakteriofagi 1031 kwenye sayari yetu, zaidi kuliko viumbe vingine vyote duniani kwa pamoja, hata pamoja na bakteria. Virusi ni viumbe vya kibiolojia vilivyo vingi kabisa katika safuwima ya maji ya bahari za dunia na sehemu kubwa ya pili ya biomasi baada ya prokarioti, ambapo hadi virioni 9*108 kwa ml zimepatikana kwenye mikeka ya vijiumbe kwenye uso wa maji, na hadi 70% ya bakteria wa baharini wanaweza kuambukizwa na fagi.
Fagi zimetumika tangu mwishoni mwa karne ya 20 kama njia mbadala ya viuavijasumu katika Umoja wa Kisovyeti wa zamani na Ulaya ya Kati na pia katika Ufaransa. Zinaonekana kama tiba inayowezekana dhidi ya aina nyingi za bakteria wenye kukinza dawa kadhaa (angalia tiba kwa fagi). Kwa upande mwingine, fagi za Inoviridae zimeonyeshwa kuimarisha bioutando zinazohusika na nimonia na uvimbe wa fibrosisi na kusitiri bakteria kutoka kwa dawa zilizokusudiwa kutokomeza magonjwa na hivyo kusababisha maambukizo yanayodumu.
© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search