Bogota


Jiji la Bogota
Nchi Kolumbia
Tovuti:  www.bogota.gov.co
Kanisa kuu la kale la Bogota

Bogota (jina kamili: Santa Fe de Bogotá) ni mji mkuu wa Kolombia pia mji mkubwa wa nchi mwenye wakazi milioni saba takriban.

Mji uko katika nyanda za juu kwenye kimo cha 2,640 m juu ya UB kati ya milima ya Guadalupe (3,317 m) na Monserrate (3,100 m).

Mji ulianzishwa na Mhispania Gonzalo Jiménez de Quesada tar. 6 Agosti 1538 kwenye mahali pa soko la Wachibcha lililoitwa "Bacata". Quesada alitumia jina la "Santa Fe" (kihisp.: "imani takatifu") kutokana na mji wa Hispania alikotokea mwenyewe.

Baadaye mji uliongezewa jina la pili "Bogota" kutokana na jina asilia "Bacata". Jina kamili lilikuwa "Santa Fe de Bogota".


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search