Bosnia na Herzegovina

Bosna i Hercegovina
Босна и Херцеговина

Bosnia na Herzegovina
Bendera ya Bosnia na Herzegovina Nembo ya Bosnia na Herzegovina
Bendera Nembo
Kaulimbiu ya taifa: --
Wimbo wa taifa: "Intermeco"
Lokeshen ya Bosnia na Herzegovina
Mji mkuu Sarajevo
43°52′ N 18°25′ E
Mji mkubwa nchini Sarajevo
Lugha rasmi Kibosnia, Kikroatia, Kiserbia
Serikali
Marais

Mwenyekiti wa
halmashauri ya mawaziri
Jamhuri
Šefik Džaferović (Mbosnia)
Milorad Dodik 1(Mserbia)
Željko Komšić (Mkroatia)
Zoran Tegeltija
Uhuru
Ilitambuliwa

6 Aprili 1992
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
51,197 km² (128)
--
Idadi ya watu
 - Julai 2006 kadirio
 - 2014 sensa
 - Msongamano wa watu
 
4,498,9762 (ya 1273)
3,871,643[1]
76/km² (ya 1163)
Fedha Convertible mark
pamoja na Euro (BAM4)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
CET (UTC+1)
CEST (UTC+2)
Intaneti TLD .ba
Kodi ya simu +387

-

1 Maraisi watatu wanaobadilishanan
2 Kadirio ya CIA World Factbook [2].



Bosnia na Herzegovina (Bosna i Hercegovina au Босна и Херцеговина) ni nchi ya Ulaya kusini mashariki kwenye rasi ya Balkani. Mara nyingi huitwa kwa kifupi "Bosnia" tu na watu wake "Wabosnia". Ilikuwa sehemu ya Yugoslavia hadi mwaka 1992.

Eneo lake ni km² 51,129 linalokaliwa na wakazi karibu milioni nne.

Mji mkuu ni Sarayevo.

Kati ya wakazi kuna vikundi vitatu vinavyotofautiana kiutamaduni na kidini: Wabosnia (48%), Waserbia (37.1%) na Wakroatia (14.3%). Wanadai ya kwamba lugha zao ni tofauti, lakini hali halisi ni lugha ileile ya Kislavoni. Wakati wa Yugoslavia iliitwa "Kiserbokroatia". Tofauti ziko kwa sababu Wabosnia hutazamiwa kuwa Waislamu, Waserbia kuwa Waorthodoksi na Wakroatia kuwa Wakristo Wakatoliki.

Nchi ina vitengo viwili: Shirikisho la Bosnia na Herzegovina linalounganisha maeneo ya Waislamu na ya Wakatoliki na Republika Srpska au eneo la Waserbia Waorthodoksi.

Ramani ya Bosnia na Herzegovina

© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search