Chuo Kikuu

Chuo Kikuu cha Bologna (Italia) kilikuwa chuo kikuu cha kwanza cha Ulaya.
Nyumba ya Hekima mjini Baghdad (Iraki) ilikuwa kati ya watangulizi wa vyuo vikuu katika dunia ya Kiislamu tangu mwaka 800 BK.

Chuo Kikuu ni taasisi ya elimu ya ngazi ya juu ambako wanafunzi wanafundishwa na wataalamu wa fani mbalimbali ambao hufundisha pamoja na kuendesha uchunguzi wa elimu mpya.

Wanafunzi husoma kwenye chuo kikuu kwa shabaha ya kupata elimu hadi kupita mitihani ya shahada au digrii kama vile ya bachelor (ya kwanza), ya uzamili (master) (ya pili) na ya uzamivu, PhD (ya tatu).


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search