Dinosauri | ||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
![]() | ||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||
| ||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||
2 Orders:
|
Dinosauri (pia: dinosau, dinosari, dinosaria kutoka maneno ya Kigiriki δεινός, deinos – "wa kutisha", σαῦρος, sauros - "mjusi") ni jina la kundi la reptilia wakubwa sana walioishi duniani miaka milioni kadhaa iliyopita.
Wataalamu huamini ya kwamba dinosauri walitokea miaka milioni 230 iliyopita wakatoweka ghafla miaka 65 iliyopita. Ndege hutazamwa kuwa katika nasaba ya dinosauri.
Ujuzi kuhusu wanyama hao unatokana na visukuku vyao (mabaki ambayo yamekuwa mawe) kama vile mifupa, nyayo, mayai au samadi. Visukuku vya dinosau vimepatikana kwenye mabara yote, hata Antaktika, kwa sababu waliishi wakati mabara yote yalikuwa bado pamoja kama bara kubwa asilia la Pangaia.
© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search