Dinosauri

Dinosauri

Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Sauropsida (Wanyama wanaofanana na watambaazi)
Nusungeli: Diapsida (Wanyama wenya mashimo mawili kando la fuyu la kichwa)
Oda ya juu: Dinosauria (Wanyama kama dinosauri)
Ngazi za chini

2 Orders:

  • Ornithischia
  • Saurischia

Dinosauri (pia: dinosau, dinosari, dinosaria kutoka maneno ya Kigiriki δεινός, deinos – "wa kutisha", σαῦρος, sauros - "mjusi") ni jina la kundi la reptilia wakubwa sana walioishi duniani miaka milioni kadhaa iliyopita.

Kulinganisha ukubwa wa tiranosauri na binadamu.

Wataalamu huamini ya kwamba dinosauri walitokea miaka milioni 230 iliyopita wakatoweka ghafla miaka 65 iliyopita. Ndege hutazamwa kuwa katika nasaba ya dinosauri.

Ujuzi kuhusu wanyama hao unatokana na visukuku vyao (mabaki ambayo yamekuwa mawe) kama vile mifupa, nyayo, mayai au samadi. Visukuku vya dinosau vimepatikana kwenye mabara yote, hata Antaktika, kwa sababu waliishi wakati mabara yote yalikuwa bado pamoja kama bara kubwa asilia la Pangaia.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search