Eneo

Maumbo matatu ya jiometria yenye maeneo tofauti (msambamba, pembetatu, duara)

Eneo katika elimu ya jiometria ni idadi inayoeleza ukubwa wa umbo bapa lenye upana na urefu. Kwa hiyo „eneo“ linataja ukubwa wa gimba lenye wanda mbili.

Hii inamaanisha maumbo ya jiografia bapa kama vile mraba, mstatili na duara lakini pia uso wa gimba lenye wanda tatu kama vile mchamrembe au tufe.

Ukubwa wa eneo linapimwa kwa kuulinganisha na miraba maalumu. Katika mfumo wa vipimo sanifu vya kimataifa kizio sanifu ni mita ya mraba (inayofupishwa kwa m²). Umbo kama mviringo mwenye eneo la 3 una eneo sawa na miraba mitatu ya aina hii.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search