Fransisko wa Asizi

Mchoro wa zamani wa Fransisko wa Asizi unaoaminiwa kufanana naye kuliko yote

Fransisko wa Asizi (kwa Kiitalia Francesco d'Assisi; tangu utotoni jina la ubatizo Giovanni, yaani Yohane (Mbatizaji), liliachwa kutumika; pia ubini mwana wa Petro Bernardone ulikuja kuachwa baada ya wao kushindana; Assisi, Italia, 1181 au 1182 - Assisi, 3 Oktoba 1226) alikuwa mtawa shemasi wa Kanisa Katoliki.

Baada ya kuishi ujana wenye raha, aliongokea maisha ya Kiinjili ili kumtumikia Yesu Kristo aliyekutana naye hasa katika watu maskini na walalahoi, akijifanya fukara vilevile, na hatimaye alitaka kufa uchi ardhini.

Akizungukazunguka huko na huko, hadi Nchi takatifu, aliwahubiria watu wa kila aina upendo wa Mungu akilenga kuiga kikamilifu kila siku mfano wa Yesu kwa maneno na matendo[1].

Alianzisha jumuiya ya kitawa yenye matawi mbalimbali ambayo leo ni utawa wenye wafuasi wengi kuliko yote wakikadiriwa kukaribia milioni moja duniani kote.

Alitangazwa na Papa Gregori IX kuwa mtakatifu tarehe 16 Julai 1228.

Anaheshimiwa na wengi hata nje ya Kanisa lake, ambalo limemtangaza [msimamizi]] wa wanaoshughulikia hifadhi ya mazingira.

Sikukuu yake inaadhimishwa tarehe 4 Oktoba[2].

  1. https://www.santiebeati.it/dettaglio/21750
  2. Martyrologium Romanum

© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search