Fueli

Ubao ulikuwa kati fueli za kwanza za binadamu

Fueli ni dutu inayowaka na kutoa nishati kwa njia inayoweza kutumiwa na binadamu. Mara nyingi fueli ni kitu kinachochomwa.

Kwa lugha ya kawaida si kila mara kikiwaka ya kwamba kinastahili kuitwa vile: ubao ukitumiwa jikoni kama kuni ni fueli; ubao ukiwaka hovyo wakati msitu inaharibika na moto si fueli.

Lakini kwa matumizi ya kitaalamu kile kinachowaka ni kampaundi za kaboni na hidrojeni ndani ya ubao na hii ni fueli yenyewe kwa maana ya kikemia.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search