Hija

Wayahudi wakisali kwenye Ukuta wa Maombolezo, Yerusalemu.
Mlango mkuu wa Kanisa la Kaburi na Ufufuo wa Yesu, Yerusalemu.
Hija ya Waislamu kwenye Masjid al-Haram, Maka, mwaka 2008.

Hija (kutoka Kiarabu حج, hajj, kitenzi kuhiji) ni ziara ya kidini yaani ni safari inayofanyika kwa sababu ya dini, ikilenga patakatifu fulani.

Kwa maana ya kiroho, maisha yote ni safari ya kumuelekea Mungu au uzima wa milele n.k.

Sababu ya kwenda mahali maalumu ni tumaini la kuwa karibu zaidi na imani mahali ambako mambo muhimu ya historia ya dini husika yalitokea; mara nyingi pia imani ya kwamba sala itakuwa na nguvu au mafanikio zaidi pale.

Desturi ya kuhiji iko katika dini mbalimbali.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search