Ijumaa Kuu

Msalaba wa Ijumaa Kuu kwenye Monasteri ya Utatu Mtakatifu, Meteora, Ugiriki.
Mwaka wa liturujia
Magharibi
Mashariki
Picha takatifu ya karne ya 16 ikionyesha tendo la kumsulubu Yesu kadiri ya Theophanes wa Krete (Stavronikita Monastery, Mlima Athos, Ugiriki).
Siku ya Ijumaa Kuu Wakatoliki wanapokea ekaristi ingawa Misa haiadhimishwi (Our Lady of Lourdes, Philadelphia, Marekani).
Njia ya Msalaba ikiadhimishwa kwenye Colosseum mjini Roma siku ya Ijumaa Kuu. Mwishoni, Papa anatoa neno.
Picha ya El Greco ikimuonyesha Yesu akibeba msalaba, 1580.
Epitafyo ya Kiorthodoksi ikionyesha mwili wa Yesu ukizikwa.
Epitafyo ikichukuliwa katika maandamano.

Ijumaa Kuu ni siku ya Ijumaa kabla ya Pasaka ambapo Wakristo wengi duniani wanaadhimisha kifo cha Yesu Kristo msalabani.

Kufuatana na taarifa za Injili nne katika Biblia ya Kikristo, Yesu alisulubiwa siku kabla ya Sabato (au Jumamosi), yaani Ijumaa. Mahali pa kumsulubisha palikuwa kilima cha Golgotha kilichokuwepo wakati ule nje ya kuta za mji wa Yerusalemu.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search