Italia

Repubblica Italiana
Jamhuri ya Italia
Bendera ya Italia Nembo ya Italia
Lugha rasmi Kiitalia; kijimbo pia Kijerumani, Kifaransa, Kiladino, Kislovenia, Kisardinia
Mji Mkuu Roma
Rais Sergio Mattarella
Waziri Mkuu Mario Draghi
Eneo km² 302,072.84
Wakazi 59,236,213 (31-12-2020) (23º duniani)
Wakazi kwa km² 201.7
JPT 31,022 US-$ (2008)
Pesa Euro
Wakati UTC+1
Wimbo wa Taifa Fratelli d'Italia (Ndugu wa Italia)
Sikukuu ya Jamhuri 2 Juni
Sikukuu ya Ukombozi 25 Aprili
Simu ya kimataifa +39
Italia katika Ulaya na katikati ya Bahari ya Kati.
Ramani ya Italia
Italia jinsi inavyoonekana kutoka angani

Jamhuri ya Italia (kwa Kiitalia: Repubblica Italiana) ni nchi ya Ulaya Kusini inayoenea katika sehemu kubwa ya Rasi ya Italia na baadhi ya visiwa vya jirani kwenye Bahari ya Kati.

Eneo lake ni km² 302,072.84 ambalo lina wakazi 59,236,213 (31-12-2020): ni nchi ya 23 duniani kwa wingi wa watu, lakini ya 8 au 9 kwa uchumi. Mtu anayetokea katika nchi hii ya Italia kwa Kiswahili huitwa Mwitalia.

Imepakana na Ufaransa, Uswisi, Austria na Slovenia. Nchi huru mbili ndogo zinazozungukwa na eneo la Italia pande zote ni San Marino na Vatikano.

Makao makuu ni jiji la Roma, lenye umuhimu mkubwa katika historia ya dunia nzima.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search