Jamhuri ya Dominika

República Dominicana
Jamhuri ya Dominika
Bendera ya Jamhuri ya Dominika Nembo ya Jamhuri ya Dominika
Bendera Nembo
Kaulimbiu ya taifa: Kihispania: Dios, Patria, Libertad
( Mungu, Taifa, Uhuru)
Wimbo wa taifa: Quisqueyanos valientes
Lokeshen ya Jamhuri ya Dominika
Mji mkuu Santo Domingo
18°30′ N 69°59′ W
Mji mkubwa nchini Santo Domingo
Lugha rasmi Kihispania
Serikali Jamhuri
Luis Abinader
Uhuru
Tarehe
27 Februari 1844
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
48,442 km² (ya 131)
1.6
Idadi ya watu
 - Julai 2020 kadirio
 - 2010 sensa
 - Msongamano wa watu
 
11,229,403 (ya 86)
9,445,281
231.81/km² (ya 65)
Fedha Peso ya Dominika (DOP)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
(UTC-4)
(UTC)
Intaneti TLD .do
Kodi ya simu +1-809 and +1-829

-


Ramani ya Jamhuri ya Dominika

Jamhuri ya Dominika ni nchi iliyoko kwenye kisiwa cha Bahari ya Karibi cha Hispaniola na inayopakana na Haiti tu.

Hispaniola ni kisiwa kikubwa cha pili cha Antili Kubwa (baada ya Kuba) na iko upande wa magharibi wa Puerto Rico, karibu na Kuba na Jamaica. Wenyeji kwa ajili ya kisiwa chao hutumia pia jina la Quisqueya ambalo ni neno la Kitaino, lugha ya wakazi asilia.

Mji mkuu na pia mji mkubwa ni Santo Domingo (yaani Mtakatifu Dominiko). Jina la nchi linatokana na hilo (Jamhuri ya Mt. Dominiko). Jina hilo wakati mwingine linachanganywa na lile la Dominica ambayo ni nchi nyingine iliyoko katika kisiwa cha Karibi chenye jina kama hilo ila lenye maana ya Siku ya Bwana, yaani Jumapili.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search