Kazi

Wachimbaji wa mfereji wa maji kwenye mto Cedar, Washington (1899).
Wanawake wengi pamoja katika kazi ya ofisini.
Mwanafalsafa kazini alivyoonyeshwa na sanamu ya August Rodin, "Le penseur" (= "Mwenye kufikiri").
Mfanyakazi akishughulikia mashine (picha ya Lewis Hine, 1920).

Kazi ni sehemu muhimu ya maisha ya binadamu, hivyo ina nafasi kubwa katika anthropolojia, falsafa, teolojia,fizikia na sosholojia.

Inafafanuliwa kama utendaji unatumia nguvu ya akili au ya mwili ili kufikia lengo fulani, ambalo mara nyingi ni faida ya kiuchumi ili kuweza na kuwezesha kuendelea kuishi.

Lakini thamani yake halisi haiishii katika uzalishaji wa vitu, bali inategemea hasa ustawishaji wa utu katika vipawa vyake vyote kulingana na maadili na maisha ya kiroho.

Kwa msingi huo, ni wajibu wa kila mtu aliyefikia ukomavu fulani.

Ni pia mchango muhimu katika jamii na inayostahili kuheshimiwa na kutunzwa na wote kuanzia serikali hadi watu binafsi.

Kwa kuwa ni wajibu, kazi ni vilevile haki ya msingi ya binadamu. Bila kuwa nayo, mtu anaelekea kunyong'onyea na kujiona hama maana, hasa kama utovu wa kazi unadumu muda mrefu na kumzuia asiweze kupanga maisha yake, kwa mfano upande wa ndoa na familia, kwa sababu ya kutojitegemea.

Sheria mbalimbali zinaratibu mahusiano kazini, hasa kama kuna mwajiri na mwajiriwa.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search