Khalifa

Eneo la utawala wa makhalifa wakati wa mwisho wa Wamuawiya mw. 750

Khalifa, ni cheo cha kihistoria kwa ajili ya kiongozi wa umma (jumuiya ya Uislamu). Ni neno la Kiarabu خليفة khalīfah linalomaanisha "makamu". Khalifa ni kifupi chake cha خليفة رسول الله "khalifatu-rasul-i-llah" kinachomaanisha "Makamu wa mtume wa Allah/Mungu". Hivyo mana yake ni makamu au mfuasi wa Mtume Muhammad katika nafasi yake kama kiongozi wa Waislamu.

Cheo cha khalifa kilitumiwa pamoja na cheo cha "amīr-al-mu'minīn" ( أمير المؤمنين ) "Jemadari Mkuu wa wenye Imani (=Waislamu)".

Utaratibu wa uongozi wa khalifa ulianzishwa baada ya kifo cha Mtume Muhammad mwaka 632 na kuishia 3 Machi 1924 katika mapinduzi ya Atatürk.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search