Kipindi cha Pasaka

Kipindi cha Pasaka katika mwaka wa Kanisa kinaonyeshwa na rangi ya njano.
Mwaka wa liturujia
Magharibi
Mashariki

Kipindi cha Pasaka ni kipindi maalumu cha mwaka wa Kanisa katika madhehebu mbalimbali ya Ukristo.

Ni kwamba Wayahudi wanaadhimisha Pasaka ya kale, ukumbusho wa kuvuka pakavu kati ya bahari, kutoka utumwani kuelekea uhuru. Kumbe Wakristo wanaadhimisha Pasaka mpya, ukumbusho wa sadaka ya Agano Jipya la milele ambayo pamoja na Yesu wanavuka toka dunia hii kwenda kwa Baba: Kristo asingefufuka imani hiyo ingekuwa bure.

Maelezo yafuatayo yanatokana na mpango wa Kanisa Katoliki, lakini kwa kiasi kikubwa yanafaa pia kwa madhehebu mengine, kama vile Anglikana.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search