Kitubio

Masanduku ya Kitubio katika Kanisa kuu la Santiago de Compostela (Hispania).


Kitubio au Upatanisho ni sakramenti ya Kikristo katika Kanisa Katoliki, Makanisa ya Kiorthodoksi na madhehebu mengine machache.

Kwa njia yake Mkristo aliyetubu anapokea kwa huduma ya Kanisa msamaha wa Mungu kwa dhambi alizotenda baada ya Ubatizo.

Kwa sababu hiyo, pamoja na Mpako wa wagonjwa ni kati ya sakramenti mbili za "uponyaji", zinazolenga afya ya roho na mwili inayoharibiwa na dhambi na ugonjwa.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search