Korintho

Mahali pa Korintho nchini Ugiriki.

Korintho (kwa Kigiriki: Κόρινθος, Kórinthos) ni mji wa Ugiriki wa Kusini. Uko kwenye shingo ya nchi ya Korintho inayounganisha rasi ya Peloponesi na sehemu kubwa ya Ugiriki bara.

Siku hizi ni mji mdogo tu, wenye wakazi 36,555, lakini ina historia kubwa na ndefu.

Kimataifa Korintho inajulikana kutokana na mfereji wa Korintho unaokata shingo ya nchi kwa urefu wa kilomita sita na kufupisha safari kutoka bahari ya Adria kuingia Mediteranea ya mashariki kwa meli ndogo na za wastani.

Mfereji wa Korintho unavyokata shingo ya nchi.

Kihistoria jina la mji linajulikana zaidi kutoka Biblia ya Kikristo, na hasa barua za Mtume Paulo kwa Wakristo mjini zinazopatikana katika Agano Jipya kama Waraka wa kwanza kwa Wakorinto (1Kor) na Waraka wa pili kwa Wakorinto (2Kor).


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search