Kristoforo Kolumbus

Kristoforo Kolumbus
Jahazi ya Santa Maria imejengwa tena kwa mfano wa jahazi ya Kolumbus miaka 500 iliyopita
Msanii alichora picha hii mwaka 1893 akitaka kumwonyesha Kolumbus jinsi alivyofika Amerika mwaka 1492
Ramani ya safari nne za Kolumbus

Kristoforo Kolumbus (kwa Kiitalia: Cristoforo Colombo; kwa Kihispania: Cristóbal Colón; kwa Kilatini: Columbus; Genova, Italia, 1451; Valladolid, Hispania, 20 Mei 1506) alikuwa mfanyabiashara na mpelelezi aliyegundua njia ya usafiri kati ya Ulaya na Amerika.

Mara nyingi aliitwa Mzungu wa kwanza wa kufika Amerika, lakini baadaye imejulikana ya kwamba Waviking walitangulia kufika Amerika ya Kaskazini mnamo mwaka 1000. Ila jitihada zake zilianzisha njia ya mawasiliano ya kudumu kati ya Amerika na mabara mengine tofauti na safari zote zilizovuka bahari kabla yake.

Upande wa dini, alikuwa Mkristo wa Kanisa Katoliki, tena mwanachama wa Utawa wa Tatu wa Mt. Fransisko.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search