Kuba (jengo)

Muundo wa kuba

Kuba (Kar. قبة kubba) ni sehemu ya jengo inayoonekana kama nusu tufe iliyoko juu ya jengo fulani.

Ni sifa inayolenga kuonyesha umuhimu maalum wa jengo hili. Hivyo ni hasa makanisa, misikiti na majengo makubwa ya serikali zinazopambwa kwa kuba juu yake. Pamoja na hayo kuba inaweza kupazia sauti ya mseamji chini yake hivyo imesaidia kwa kusudi la kuwahotubia watu wengi.

Kati ya Waswahili wa Afrika ya Mashariki kuna desturi ya kupamba makaburi ya watu muhimu kama mashehe kwa kujenga kuba juu yake.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search