Majimbo ya Afrika Kusini

Majimbo ya Afrika Kusini

Majimbo ya Afrika Kusini ni ngazi ya kwanza ya ugatuzi nchini Afrika Kusini. Nchi imegawanywa katika majimbo tisa. [1] Katika mkesha wa uchaguzi mkuu wa 1994 nchi ilikuwa na majimbo manne halafu kulikuwa na maeneo ya bantustan. Kabla ya uchaguzi huo wa kwanza ulioendeshwa bila ubaguzi wa rangi maeneo ya bantustan yaliunganishwa tena kisheria na Afrika Kusini na nchi yote iligawiwa kwa majimbo tisa.

  1. "The nine provinces of South Africa - South Africa Gateway", South Africa Gateway, 2018-04-06. 

© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search