Makaburu

Jan van Riebeeck na wenzake wakifika Afrika Kusini, mchoro wa Charles Bell.

Makaburu (kutoka Kiholanzi na Kiafrikaans boer inayomaanisha mkulima) ni jina la walowezi Wazungu wa Afrika Kusini na Namibia wanaotumia lugha ya Kiafrikaans. Wenyewe wanajiita mara nyingi Afrikaner yaani "Waafrika".

Wako takriban theluthi mbili ya Wazungu wa Afrika Kusini au milioni 1.5. Karibu wote ni Wakristo Waprotestanti hasa wa madhehebu ya Kikalvini.

Baada ya kushindwa katika vita vya pili vya Makaburu dhidi ya Uingereza mwaka 1902, tena baada ya mwisho wa siasa ya apartheid, vikundi vya Makaburu walihamia nje ya nchi kwenda nchi nyingine za Afrika na pia za Amerika.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search