Mawasiliano

Alama ya mawasiliano ya simu

Mawasiliano kwa kawaida hufafanuliwa kama kupashana au kubadilishana mawazo, maoni, hisia au habari kwa maneno, maandishi au ishara kufikia lengo lililokubaliwa au mwelekeo uliokubaliwa (habari)[1].

Ingawa kuna mawasiliano ya njia moja, mawasiliano yanaweza kueleweka vyema kama mchakato wa kuhamisha taarifa kati ya wahusika wawili.

Katika mawasiliano habari hupakiwa na kutumwa na kupashwa na mtu kwa anayepokea kupitia njia maalum. Kisha anayepokea hupakua ujumbe ule na kumpatia aliyetuma (ma)jibu. Aina zote za mawasiliano huhitaji mtumaji, ujumbe na mpokeaji.

Mawasiliano huhitaji kwamba wanaohusika wawe na jambo linalowaunganisha. Kuna njia zinazohusisha kusikia, kama vile unenaji, wimbo, na toni ya sauti, na kuna zile zisizohusisha kusikia, kama vile miondoko ya mwili, lugha ishara, kugusa, kuwasiliana kwa macho na kuandika.

  1. Schwartz, Gary E.; Simon, William L.; Carmona, Richard (2008). The Energy Healing Experiments. Simon & Schuster. uk. 129. ISBN 0743292399. All communication is a process of exchanging energy and exchanging information. {{cite book}}: Check |isbn= value: checksum (help)

© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search