Meli

Meli kubwa ya shehena ya mafuta ya petroli.
Muundo wa meli ya kisasa.
Jahazi.

Meli ni chombo kikubwa cha kusafiria kwenye maji.

Siku hizi meli huwa na bodi ya chuma ikisogezwa kwa nguvu ya injini inayochoma diseli.

Hadi karne ya 19 meli zilijengwa kwa kutumia mbao zikasongezwa hasa kwa nguvu ya upepo kwa kutumia tanga. Jahazi ziko hadi leo.

Meli hutumiwa hasa kwa kubeba mizigo na abiria. Kuna pia meli za kijeshi zinazoitwa manowari.

Kuna njia mbalimbali za kutofautisha ukubwa wa meli: njia ya kawaida imekuwa tani GT inayotaja mjao wa chombo.

Mkuu na kiongozi kwenye meli anaitwa nahodha. Watu wanaofanya kazi kwenye meli kwa jumla ni mabaharia.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search