Mizimu

Mizimu inamaanisha hasa roho zilizoishi katika mwili kabla ya kuiaga dunia.

Katika baadhi ya dini na mila inaaminika kuwa mizimu inaweza kuwa na faida kwa watu walio hai duniani na ina uwezo wa kuwasiliana nao kwa kutumia njia mbalimbali kufuatana na mazingira au utamaduni.

Kuna tofauti kati ya mizimu; pengine ni roho za binadamu ambao hawakutimiza majukumu yao au walifanya kinyume wakati wapo duniani; pengine ni roho za watu walioshi kwa uadilifu.

Katika Kanisa Katoliki na baadhi ya madhehebu mengine, mizimu inaweza kuwa ya watakatifu.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search