Msumbiji

República de Moçambique
Jamhuri ya Msumbiji
Bendera ya Msumbiji
Lugha ya taifa Kireno
Mji Mkuu Maputo
Aina ya Serikali Jamhuri
Rais Filipe Nyusi
Waziri Mkuu Adriano Maleiane
Eneo km² 801.590
Wakazi 31,693,239 (Julai 2022)
Wakazi kwa km² 28.7
JPT/ Mkazi 233 US-$ (2004)
Uhuru kutoka Ureno tar. 25 June 1975
Pesa Metical (MZM)
Wakati UTC +2h
Wimbo wa Taifa Pátria Amada (kwa Kireno: Nchi pendwa)
Namba ya simu ya kimataifa +258
Msumbiji katika Afrika
Msumbiji katika Afrika

Msumbiji (kwa Kireno: Moçambique) ni nchi ya Afrika ya Kusini-Mashariki.

Msumbiji iko ufukoni mwa Bahari Hindi ikipakana na Tanzania, Malawi, Zambia, Zimbabwe, Afrika Kusini na Eswatini.

Upande wa mashariki kuna kisiwa cha Madagaska ng'ambo ya mlango bahari wa Msumbiji.

Jina la nchi limetokana na Kisiwa cha Msumbiji (kwa Kireno: Ilha de Moçambique) kilichokuwa boma na makao makuu ya Ureno kwenye pwani ya Afrika ya Mashariki.

Sikukuu ya Taifa ni tarehe 25 Juni, ulipopatikana na uhuru mwaka 1975.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search