Mitume wa Yesu |
---|
|
Sehemu ya mfululizo kuhusu |
Ukristo |
---|
|
|
Simoni Petro alikuwa Myahudi wa karne ya 1, mfuasi wa Yesu Kristo, tena kati ya wandani wake.
Baada ya Yesu, ndiye mtu anayejulikana zaidi katika Injili zote nne.
Katika orodha zote nne za mitume 12 wa Yesu zinazopatikana katika Biblia ya Kikristo anashika nafasi ya kwanza (tofauti na wenzake wengi ambao wanabadilishana nafasi, na kinyume cha Yuda Iskarioti, msaliti anayepewa daima nafasi ya mwisho); isitoshe Math 10:2 inasisitiza nafasi yake hiyo: "Wa kwanza Simoni aliyeitwa Petro".
Tangu kale Wakristo wengi, hasa Wakatoliki na Waorthodoksi, wanamheshimu kama mtakatifu, tena kama papa wa kwanza wa Roma hadi kifodini chake kati ya miaka 64 na 67, wakati wa dhuluma ya Dola la Roma dhidi ya Ukristo iliyoanzishwa na Kaisari Nero.
Sikukuu yake inaadhimishwa kila tarehe 29 Juni pamoja na ya Mtume Paulo[1].
© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search