Mtume Thoma

Kifodini cha Mtume Thomas kilivyochorwa na Peter Paul Rubens.
Mitume wa Yesu
Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu
Yesu
Yesu Kristo na Ukristo

Umwilisho  • Utoto wa Yesu  • Ubatizo
Arusi ya Kana • Utume wa Yesu • Mifano ya Yesu  • Miujiza ya Yesu
Kugeuka sura • Karamu ya mwisho • Msalaba wa Yesu  • Maneno saba
Kifo cha Yesu  • Ufufuko wa Yesu
Kupaa mbinguni  • Ujio wa pili
Injili  • Majina ya Yesu katika Agano Jipya  • Yesu kadiri ya historia  • Tarehe za maisha ya Yesu • Kristolojia

Mazingira ya Yesu

Wayahudi • Kiaramu • Bikira Maria • Yosefu (mume wa Maria) • Familia takatifu • Ukoo wa Yesu • Ndugu wa Yesu • Yohane Mbatizaji

Mitazamo juu ya Yesu

Mitazamo katika Agano Jipya · Mitazamo ya Kikristo • Mitazamo ya Kiyahudi • Mitazamo ya Kiislamu • Yesu katika sanaa

Thoma (au Didimo, yaani Pacha) alikuwa Myahudi wa karne ya 1, mmojawapo kati ya Mitume wa Yesu anayeheshimiwa kama mtakatifu, kwa namna ya pekee na Wakristo wa maeneo yaliyokuwa mashariki kwa Dola la Roma, kuanzia Iraq hadi India.

Inawezekana kwamba sababu yake ni kazi za utume alizozifanya huko hadi kifodini chake huko Chennai mwaka 72 (kaburi lake huonyeshwa katika mji huo wa Tamil Nadu). Mpaka leo kusini-magharibi mwa Bara Hindi wako wanaojiita "Wakristo wa Thoma" ambao kwa muda mrefu walikosa mawasiliano na Wakristo wengine wa mbali.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki, Waorthodoksi na madhehebu mengine mbalimbali kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa kila mwaka tarehe 3 Julai[1].

  1. Martyrologium Romanum

© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search