Ngozi

Kwa maana nyingine ya neno hili linganisha ngozi (maana)

Ngozi ya mkono wa binadamu.

Ngozi ni ganda la nje linalofunika mwili wa mnyama au binadamu. Aina mbalimbali huwa na aina za ngozi tofautitofauti kulingana na mazingira wanapoishi na ukoo wa spishi mbalimbali.

Ni wanyama wa nusufaili ya vetebrata pekee wenye ngozi; wengine kama konokono, kaa au wadudu huwa na kiunzi nje, si ngozi. Mamalia wote walio sehemu ya vetebrata huwa na nywele angalau chache kwenye ngozi yao.

Ngozi ikiondolewa mwilini na kushughulikiwa kwa kuikausha na kutia dawa mbalimbali inaweza kutunzwa na kutumiwa kwa kutengeneza viatu, mavazi n.k.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search