Nuhu

Sadaka ya Nuhu ilivyochorwa na Daniel Maclise.

Nuhu anajulikana na kuheshimiwa katika dini ya Uyahudi, Ukristo na Uislamu kama mfano wa mwadilifu aliyeokolewa na Mungu katika safina wakati wa gharika kuu. Kadiri ya Biblia aliishi huko Mesopotamia.

Jina lake (kwa Kiebrania נח Noah, kwa Kiarabu نوح Nuhu) linatafsiriwa na Kitabu cha Mwanzo Mfariji, lakini maana ya hakika zaidi ni Anayeendeleza ubinadamu baada ya gharika.

Anaheshimiwa kama mtakatifu. Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 18 Novemba.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search