Ono

Ono.

Ono ni hali inayompata binadamu au mnyama kwa ndani, lakini inajitokeza kwa nje (inaonekana). Ni tofauti na hali ya makusudi, kwa kuwa linasababishwa na jambo fulani. Ndiyo maana katika Kiingereza linaitwa passion, neno la mkopo kutoka lile la Kilatini passio linalotokana na kitenzi patior (kupatwa). Si lazima ono liwe hai, kali na tawala.

Maono ni mbalimbali, lakini yale ya msingi ni:

  • upande mmoja pendo (kwa jambo fulani), linalosababisha hamu (ya jambo hilo) na hatimaye furaha (jambo likipatikana); upande huo pengine kuna tumaini na ujasiri;
  • upande mwingine chuki (kwa jambo fulani), linalosababisha hofu (ya jambo hilo), hasira (dhidi ya hilo) na hatimaye huzuni (jambo likipatikana); upande huo pengine kuna hali ya kukata tamaa.

Kwa msingi huo, Thoma wa Akwino alifafanua ono kama “badiliko la hisi linalotokana na kukabili jema au baya la kihisi na linaloendana na tukio la kimwili katika muundo wake, k.mf. pigo la moyo”. Mabadiliko ya utashi ni ya roho tu, kumbe ono linaendana daima na tukio la kimwili kwa sababu hisi zinaendana na viungo.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search