Pembe (jiometria)

Pembe

Pembe ni nafasi kati ya mistari miwili pale ambako inakutana. Mistari huitwa "mikono" ya pembe. Nukta inapokutana ni kipeo au ncha.

Kiwango cha pembe hutajwa mara nyingi kwa nyuzi (alama °). Kiwango cha duara ni 360°. Jumla ya pembe katika pembetatu ni 180°.

Kuna pia vipimo vingine vya kutaja kiwango cha pembe kama vile radiani au gon.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search