Safina

Safina ya Noah (1846), mchoro wa Edward Hicks.

Safina ya Noah (kutoka Kiarabu: سفينة نوح‎, Safina Nuh; kwa Kiebrania ni: תיבת נח‎, Tevat Noaḥ) ni chombo kikubwa ambamo, kadiri ya simulizi la Kitabu cha Mwanzo (Biblia), Noah na familia yake walikombolewa wakati wa gharika kuu.

Pamoja nao wanyama wa kila aina waliokolewa humo wasife maji.

Kadiri ya kitabu hicho cha Agano la Kale, sura 6-9, Mungu ndiye aliyemuagiza Noah atengeneze chombo hicho.

Habari hiyo inapatikana pia, kwa tofauti kadhaa, katika Quran.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search