Samaki

Kuhusu kundinyota la Pisces linaloitwa pia "Samaki" angalia hapa

Samaki
Kundi la tengesi mkia-njano (Sphyraena flavicauda)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Faila ya chini: Gnathostomata (Wanyama wenye mataya)
Ngazi za chini

Kladi 5 za samaki:

Papa buluu.

Samaki ni wanyama wenye damu baridi wanaoishi kwenye maji ya mito, mabwawa, maziwa au bahari.

Wote ni vertebrata, yaani huwa na uti wa mgongo.

Wanatumia oksijeni iliyomo ndani ya maji kwa kuyavuta kwenye mashavu yao.

Kuna aina nyingi za samaki wadogo wenye urefu wa sentimita moja na wakubwa wenye urefu hadi mita 15. Ila tu viumbehai wakubwa kwenye maji si samaki bali nyangumi ambao ni mamalia.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search