Shirikisho la Mataifa

Nyumba ya Mataifa huko Geneva, Uswisi ilijengwa 1929 - 1938 kama makao makuu ya Shirikisho la Mataifa. Leo ni makao makuu ya UM katika Ulaya.

Shirikisho la Mataifa (kwa Kiingereza: League of Nations) lilikuwa umoja wa madola 63 ya dunia kati ya 1920 na 1946 BK.

Umoja huo ulianzishwa na mataifa washindi wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia. Katika miaka 1920-1930 mataifa mengine yalijiunga nao.

Shirikisho la Mataifa lilikwisha 1946 baada ya kuundwa kwa Umoja wa Mataifa iliochukua nafasi yake.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search