Sifa nne za Kanisa


Sifa nne za Kanisa, kadiri ya imani ya madhehebu mengi ya Ukristo, ni zile ambazo zinalitambulisha Kanisa la kweli kati ya makundi mengi ya Ukristo ni kuwa moja, takatifu, Katoliki, la Mitume.

Sifa hizo zilitajwa na Mtaguso wa kwanza wa Konstantinopoli (381) uliporefusha Kanuni ya Imani iliyotungwa na Mtaguso wa kwanza wa Nisea (325).

Ndiyo sababu zinakubaliwa na madhehebu mengi, ingawa zinatafsiriwa nayo kwa namna tofautitofauti.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search