Televisheni

TV ya Kijerumani ya mwaka wa 1956.

Televisheni (kifupi: TV) au runinga ni chombo (kifaa) chenye skrini (kioo) ambacho kinapokea mawasiliano kutoka kituo cha televisheni na kuyabadilisha kuwa picha na sauti.

Neno "televisheni" linatokana na maneno mawili: tele (kutoka Kigiriki: kwa mbali sana) na visio (kutoka Kilatini: mwono; kwa pamoja yanaunda neno la Kiingereza television lililotoholewa katika Kiswahili televisheni.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search