Ucheki

Česká republika
Jamhuri ya Kicheki
Bendera ya Ucheki, Czech Nembo ya Ucheki, Czech
Bendera Nembo
Kaulimbiu ya taifa: Pravda vítězí
(Kicheki: "Ukweli hushinda")
Wimbo wa taifa: Kde domov můj
Lokeshen ya Ucheki, Czech
Mji mkuu Praha
50°05′ N 14°28′ E
Mji mkubwa nchini Praha
Lugha rasmi Kicheki
Serikali Jamhuri
Petr Pavel
Petr Fiala
'
Kutokea kwa taifa
Uhuru
kutoka Austria-Hungaria
Mwisho wa Chekoslovakia

Karne ya 9 (Dola la Moravia)
28 Oktoba 1918

1 Januari 1993
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
78,866 km² (ya 117)
2.0
Idadi ya watu
 - 2023 kadirio
 - 2021 sensa
 - Msongamano wa watu
 
10,827,529 (ya 85)
10,524,167
133/km² (ya 91)
Fedha Koruna (CZK)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
CET (UTC+1)
CEST (UTC+2)
Intaneti TLD .cz 3
Kodi ya simu +4201



Ramani ya Ucheki

Ucheki au Chekia au Czechia (kwa Kicheki: Česko) pia Jamhuri ya Kicheki au Jamhuri ya Czech (kwa Kicheki: Česká republika) ni nchi ya Ulaya ya Kati na mwanachama wa Umoja wa Ulaya.

Imepakana na Poland, Ujerumani, Austria na Slovakia.

Mji mkuu ni Praha (Kijer.: Prag; Kiing.: Prague).

Miji mingine mikubwa ni Brno, Ostrava, Zlín, Plzeň, Pardubice, Hradec Králové, České Budějovice, Liberec, Olomouc na Ústí nad Labem.

Tangu zamani nchi imekuwa na kanda za Bohemia, Moravia na Silesia.

Wakazi husema hasa Kicheki ambacho ni lugha ya Kislavoni ya Magharibi.

Ni kati ya nchi ambako dini si muhimu kimaisha. Wakati wa sensa ya mwaka 2021, 56.9% ya wakazi walisema hawana dini yoyote, 30.1% hawakujibu swali husika, 11.7% walijitambulisha kama Wakristo (Wakatoliki 9.3% na madhehebu mengine 2.4%).


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search