Umoja wa Ulaya

Umoja wa Ulaya
Kibulgaria: Европейски съюз
Kicheki: Evropská unie
Kidenmark: Den Europæiske Union
Kieire: An tAontas Eorpach
Kiestonia: Euroopa Liit
Kifaransa: Union européenne
Kifini: Euroopan unioni
Kigiriki: Ευρωπαϊκή Ένωση
Kihispania: Unión Europea
Kiholanzi: Europese Unie
Kihungaria: Európai Unió
Kiingereza: European Union
Kiitalia: Unione Europea
Kijerumani: Europäische Union
Kikroatia: Europska unija
Kilatvia: Eiropas Savienība
Kilituanya: Europos Sąjunga
Kimalta: Unjoni Ewropea
Kipoland: Unia Europejska
Kireno: União Europeia
Kiromania: Uniunea Europeană
Kislovakia: Európska únia
Kislovenia: Evropska Unija
Kiswidi: Europeiska unionen
www.europa.eu

Umoja wa Ulaya (kifupisho: EU) ni muungano wa kisiasa na wa kiuchumi wa nchi 27 za Ulaya, baada ya Ufalme wa Muungano kujitoa tarehe 31 Januari 2020, tukio la kwanza la namna hiyo.

Ulianzishwa mwaka 1991 juu ya msingi wa Jumuiya ya Kiuchumi ya Ulaya.

Shabaha kuu zilikuwa kujenga uchumi wa pamoja, kuboresha maisha ya watu wa Ulaya na kuzuia vita kati ya nchi za Ulaya.

Nchi 19 za Umoja huo hutumia pesa moja ya Euro.

Nchi nyingi za Umoja zimepatana kufungua mipaka yao bila vizuizi kwa wakazi wote.

European Commission (Brussels)

© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search