Vatikani

Uwanja wa Mt. Petro ni sehemu ya Mji wa Vatikani; majengo mengine karibu yote yanayoonekana pichani ni sehemu ya Italia tayari.
Status Civitatis Vaticanae
Stato della Città del Vaticano

Dola la Mji wa Vatikani
Bendera ya Vatikani Nembo ya Vatikani
Bendera Nembo
Kaulimbiu ya taifa:
Wimbo wa taifa: Inno e Marcia Pontificale (Kiitalia)
Wimbo la Papa
Lokeshen ya Vatikani
Mji mkuu Mji wa Vatikani1
41°54′ N 12°27′ E
Mji mkubwa nchini Mji wa Vatikani
Lugha rasmi Kilatini2, Kiitalia
Serikali Ufalme
Papa Fransisko
Pietro Parolin
Uhuru
Mkataba wa Laterani

11 Februari 1929
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
0.44 km² (ya 232)
Idadi ya watu
 - 2008 kadirio
 - Msongamano wa watu
 
791 (ya 229)
1,780/km² (ya 6)
Fedha Euro (€)4 (EUR)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
CET (UTC+1)
CEST (UTC+2)
Intaneti TLD .va
Kodi ya simu +395

-


Ramani ya Mji wa Vatikani

Mji wa Vatikani ni dola-mji lenye eneo la kilomita za mraba 0,44 tu. Hivyo ni nchi ndogo kuliko zote duniani. Pande zote inazungukwa na Italia.

Idadi ya wakazi ni 791; raia ni 565 tu (mnamo Oktoba 2008).

Ni nchi ya Papa ambaye ni askofu wa Roma na mkuu wa Kanisa Katoliki duniani kote.

Jina limetokana na kilima cha Vatikani (kwa Kilatini: Mons Vaticanus) ndani ya jiji la Roma, upande wa magharibi wa mto Tiber.

Pamoja na Basilika la Mt. Petro, jengo la kanisa kubwa kuliko yote duniani, Vatikani ina makanisa mengine saba, jumba la Vatikani, ofisi za utawala wa Kanisa Katoliki, mabustani, stesheni ya treni, nyumba za kuishi, hosteli kwa ajili ya mafukara na makumbusho yenye hazina kubwa za sanaa kiasi kwamba nchi nzima inahesabiwa na UNESCO kuwa Urithi wa dunia (tangu mwaka 1984).


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search