Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia

Shirikiano za kijeshi katika Ulaya mwaka 1915. Nyekundu: Mataifa ya Kati; kijani: Mataifa ya Ushirikiano; njano: mataifa yasiyoshiriki vita
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia: <br />1.Mifereji huko Verdun (Ufaransa) baada ya kulimwa kwa mizinga mikubwa; <br />2. Ndege za kijeshi na faru za kwanza; <br />3. bunduki ya mtombo na manowari
Ramani ya dunia ikionyesha nchi na maeneo yaliyoshiriki katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia. Kijani: Mataifa ya Ushirikiano; njano: Mataifa ya Kati ; nchi zisizoshiriki kwa rangi ya kijivu

Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia ilikuwa vita iliyopigwa kuanzia mwaka 1914 hadi 1918. Mataifa wapiganaji yalikuwa Ujerumani, Austria-Hungaria, Bulgaria na Uturuki (ziliitwa "Mataifa ya Kati", ing. central powers) kwa upande mmoja dhidi ya Ufaransa, Urusi, Uingereza, Italia, Marekani na nchi mbalimbali zilizoshirikiana nazo (zilitwa "Mataifa ya Ushirikiano", ing. allied powers).

Vita hii ilianza katika Ulaya ikapanuka haraka hadi Mashariki ya Kati. Kupitia koloni za Ujerumani ilipiganiwa pia Afrika na Asia ya Mashariki ikasababisha kifo cha takriban watu milioni tisa.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search