Volkswagen

Volkswagen logo 2019-present
Kiwanda cha viwanda cha Volkswagen huko Wolfsburg, kilichoonyeshwa mnamo 2006
Nchi penye viwanda vya makampuni chini ya VW duniani

Volkswagen (maana ya Kijerumani: gari la wananchi) inayojulikana pia kwa kifupi chake VW (tamka ing. vii-dabl-yu au jer. vau-we) ni kampuni ya kutengeneza motokaa kutoka nchini Ujerumani. Makao makuu yapo mjini Wolfsburg katika jimbo la Saksonia Chini lakini ina viwanda katika sehemu nyingi za Ujerumani na nchi nyingi hadi Afrika, Asia na Amerika.

Kampuni ya Volkswagen ni pia mwenye makampuni ya Audi, Bentley, Bugatti, Lamborghini, Seat, Škoda na Scania. Ni kampuni kubwa ya kutengeneza magari katika Ulaya na ya tatu duniani. Imetangaza ya kwamba inalenga kuwa kampuni kubwa ya kutengeneza magari duniani kabisa.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search