Washia

Nchi za Waislamu wengi na madhehebu
Kibichi: Wasunni wengi; Nyekundu: Washia wengi
Sehemu ya mfululizo wa makala juu ya

Uislamu

Imani na ibada zake

Umoja wa Mungu
Manabii
Misahafu
Malaika
Uteule
Kiyama
Nguzo za Kiislamu
ShahadaSwalaSaumu
HijaZaka

Waislamu muhimu

Muhammad

Abu BakrAli
Ukoo wa Muhammad
Maswahaba wa Muhammad
Mitume na Manabii katika Uislamu

Maandiko na Sheria

Qur'anSunnahHadithi
Wasifu wa Muhammad
Sharia
Elimu ya Sheria za KiislamuKalam

Historia ya Uislamu

Historia
SunniShi'aKharijiyaRashidunUkhalifaMaimamu

Tamaduni za Kiislamu

ShuleMadrasa
TauhidiFalsafaMaadili
Sayansi
SanaaUjenziMiji
KalendaSikukuu
Wanawake
ViongoziSiasa
Uchumi
UmmaItikadi mpyaSufii

Tazama pia

Uislamu na dini nyingine
Hofu ya Uislamu

Washia (pia: Shi'a; kutoka Kiarabu:شيعة[1]) ni dhehebu katika Uislamu (Kiarabu: الإسلام). Kufuatana na makadirio mbalimbali kati ya asilimia 10 na 20 za Waislamu wote hufuata Shia na wengine walio wengi ni Wasunni.

Lakini katika nchi za Uajemi, Azerbaijan, Iraki, Bahrain, Yemen, Omani na Lebanoni Washia ndio kundi kubwa.

Tofauti kubwa kati ya madhehebu mawili hayo ni juu ya suala la uimamu au ukhalifa baada ya Mtume; hata hivyo, wana tofauti juu ya masuala mengine ya kiitikadi na hukumu pia.

Waislamu wa shia wanaamini kwamba hakuna uwongo au makosa katika Qur'an na imebakia bila kubadilika tangu kuteremshwa kwake. Hadithi inajumuisha hotuba na matendo ya Mtume na Maimamu yanayopitishwa kwetu kwa njia ya maandishi kutoka kizazi kimoja hadi kingine.

Neno Shia linatokana na Kiarabu shiá't ali (شیعته علی) yaani "chama cha Ali" likimaanisha kundi la wafuasi wa Ali ibn Abu Talib aliyekuwa mkwe wake Mtume Muhammad na familia yake. Dhehebu hili linashikilia na kuamini kwamba Mtume alimteua Ali kama Wasii wake (Khalīfa) na Uimamu (mafundisho ya Shia) (kiongozi wa kiroho na kisiasa) baada yake.[2] Uteuzi huo ulifanyika katika tukio la Ghadir Khumm, lakini alizuiwa kumrithi Muhammad kama kiongozi wa Waislamu kama matokeo ya chaguo lililofanywa na baadhi ya masahaba wengine wa Muhammad (ṣaḥāba) pale Saqifah.

Mtazamo huo kimsingi unapingana na ule wa Uislamu wa Kisunni, ambao wafuasi wake wanaamini kwamba Muhammad hakuteua mrithi kabla ya kifo chake na wanamchukulia Abu Bakr, ambaye aliteuliwa kuwa khalifa na kundi la Waislamu wakuu pale Saqifah, kuwa khalifa wa kwanza halali (rāshidūn) baada ya Muhammad.[3]

  1. "Sunnis and Shia: Islam's ancient schism", BBC News, 2016-01-04. (en-GB) 
  2. Olawuyi, Toyib (2014). On the Khilafah of Ali over Abu Bakr. uk. 3. ISBN 978-1-4928-5884-3. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 22 Aprili 2016.{{cite book}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  3. "The Shura Principle in Islam – by Sadek Sulaiman". www.alhewar.com. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 27 Julai 2016. Iliwekwa mnamo 18 Juni 2016.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)

© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search