Yohane Mbatizaji

Yohane akimbatiza Yesu (mchoro kutoka Ufaransa mnamo karne ya 15).

Yohane Mbatizaji (7 K.K. - 29 B.K. hivi) alikuwa nabii wa Uyahudi aliyeishi wakati wa Yesu wa Nazareti na kumtangulia miezi tu kuzaliwa, kuanza utume na kuuawa.

Kufuatana na Injili ya Luka sura 1-2 Yohane na Yesu walikuwa ndugu na mama zao walikuwa wazito kwa wakati mmoja.

Habari zake zinapatikana katika Biblia ya Kikristo na katika vitabu vya mwanahistoria Yosefu Flavius.

Anaheshimiwa na Wakristo na Waislamu kama nabii na mtakatifu.

Pengine sikukuu yake muhimu zaidi ni ile ya kuzaliwa [1] (inayoadhimishwa na Kanisa la magharibi tarehe 24 Juni [2], miezi sita kabla ya Krismasi), lakini ipo pia sikukuu ya kifodini chake [3] tarehe 29 Agosti [4].

  1. https://www.santiebeati.it/dettaglio/20300
  2. Martyrologium Romanum
  3. https://www.santiebeati.it/dettaglio/24300
  4. Martyrologium Romanum

© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search