Alhaji

Alhaji (Ar. الحاجّ; pia: hujaji) au hajja kwa wanawake ni neno la kumtaja Mwislamu aliyetimiza safari ya hajj. Haikubaliki kwa mtu yeyote aliyefika Makka lakini kwa hao pekee waliofanya hija hii wakati wa siku maalumu kwenye mwezi wa Dhul-hijja na kutekeleza ibada zote zinazotakiwa.

Alhaji hutumiwa pia kama cheo cha heshima na kuwa kama sehemu ya jina la mtu.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search