Aljeri








Jiji la Aljeri

Nembo
Nchi Aljeria
Jimbo Jimbo la Aljeri

Aljeri (Kiarabu: مدينة الجزائر, madīnat al-djazā'ir, "mji wa visiwa"; Kifaransa: Alger) ni mji mkuu pia mji mkubwa kabisa wa nchi ya Aljeria ikiwa na wakazi milioni 2 (mwaka 2005), pamoja na mitaa ya nje takriban milioni 5. Iko mwambaoni mwa bahari ya Mediteranea.

Aljeri ni makao ya serikali na kitovu cha uchumi, biashara, utamaduni na mawasiliano nchini.

Kasbah yake imeorodheshwa na UNESCO kama Urithi wa Dunia.

Waingereza walivamia meli za maharamia Aljeri mnamo Agosti 1816.
Majengo ya nyakati za ukoloni.
Mtaa wa Aljeri mwambaoni.
Uwanja wa "Mashahidi wa Uhuru".
Algiers inavyoonekana kutoka angani.
Aljeri inavyoonekana kutoka angani.

© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search