Binadamu

Binadamu

Uainishaji wa kisayansi
Domeni: Eukaryota
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Mamalia (Wanyama wenye viwele wanaonyonyesha wadogo wao)
Oda: Primates (Wanyama wanaofanana kiasi na binadamu)
Familia ya juu: Hominoidea (Wanyama kama binadamu)
Familia: Hominidae (Walio na mnasaba na binadamu)
Nusufamilia: Homininae (Wanaofanana sana na binadamu)
Jenasi: Homo
Linnaeus, 1758
Spishi: H. sapiens
Linnaeus, 1758
Nususpishi: H. s. sapiens
Mchoro wa uenezi wa jenasi Homo katika miaka milioni mbili ya mwisho. Rangi ya samawati Inaonyesha uwepo wa spishi fulani wakati na mahali fulani.[1]
Ramani ya uenezi wa binadamu ([ka] inamaanisha miaka elfu).

Binadamu (pia mwanadamu[2]) ni neno lenye asili ya Kiarabu linalomaanisha "Mwana wa Adamu", anayeaminiwa na dini za Uyahudi, Ukristo na Uislamu kuwa ndiye mtu wa kwanza.

  1. Stringer, C. (2012). "What makes a modern human". Nature. 485 (7396): 33–35. doi:10.1038/485033a. PMID 22552077.
  2. Maneno "Binadamu" na "Mwanadamu" ni maneno mawili yaliyo tofauti kimatamshi lakini yenye maana moja kidhana. Neno "Binadamu" kietimolojia huundwa na maneno mawili tofauti ambayo hutokana na lugha ya Kisemiti katika lahaja za Kiarabu na Kiebrania ambapo neno "Bin" etimolojia yake ni lugha ya Kiarabu ambapo neno hilo Bin humaanisha "Mtoto wa jinsia ya kiume". Halikadhalika neno "Adamu" etimolojia yake ni kutoka katika lugha ya Kiebrania ambapo neno hilo Adamu hutokana na neno "Adamah" lenye maana ya "Ardhi". Kwa upande mwingine neno "Mwanadamu" huundwa kutokana na etimolojia mbili tofauti kutoka katika lugha za Kiswahili na Kiebrania ambapo katika etimolojia ya lugha ya Kiswahili hutoka neno "Mwana" ambalo humaanisha "Mtoto" na ambapo pia etimolojia yake hutoka katika neno la Kibantu "Omona/Umwana" lenye maana ya "Mtoto wa jinsia ya kiume au kike". Hivyo basi, kietimolojia inaposemwa "Bin-Adamu" humaanishwa "Mtoto wa jinsia ya kiume wa kiumbe hai yeyote mwenye asili ya ardhi" yaani "Adamah", na halikadhalika inaposemwa "Mwana-Adamu" humaanishwa "Mtoto wa jinsia ya kiume au kike aliyetokana na kiumbe hai yeyote mwenye asili ya udongo".

© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search